021surah
Tarjuma ya
Ali Muhsin Al-Barwani (Badilisha)
Taarifa ya Sura

١

IMEWAKARIBIA watu hisabu yao, nao wamo katika mghafala wanapuuza.
٢
Hayawafikilii mawaidha mapya kutoka kwa Mola wao Mlezi ila huyasikiliza na huku wanafanya mchezo.
٣
Zimeghafilika nyoyo zao. Na wale walio dhulumu hunong'onezana kwa siri: Ni nani ati huyu isipo kuwa ni binaadamu tu kama nyinyi! Mnauwendea uchawi hali nanyi mnaona?
Notes placeholders